20th Anniversary Banner

 
 

Press Release

EAC Secretariat urges Partner States to prepare economic recovery plans for the time after COVID-19

East African Community Headquarters, Arusha, Tanzania, 14 April 2020: The COVID-19 global pandemic is not only a major health crisis that challenges health systems across the globe. It has far reaching ramifications on economies worldwide. The medium- and long-term effects resulting from the measures taken to slow down and contain the spread of the disease remain unforeseeable.

The East African Community region is no exception. On a positive note, the free movement of goods and services in the EAC has been maintained and the supply situation for staple food and basic necessities is currently secured. However, on the negative side, enterprises across sectors including the agro-industry and particularly the informal sector are suffering. Value chains have been disrupted and tourism, a major source of income in the region, has come to a complete stand-still.

Continue Reading

26th Commemoration of the Genocide Against the Tutsi at EAC

East African Community Headquarters, Arusha, Tanzania, 6th April, 2020As you are aware, the People of the Republic of Rwanda and the International Community, commemorates the 1994 Genocide against the Tutsi in Rwanda every 7th of April.

We wish however to inform you that owing to the underway COVID-19 Pandemic coupled with Kwibuka26 guidelines from the Government of Rwanda and EAC guidance on public gatherings during this Corona Crisis, this year we will not have at EAC Headquarters the usual physical commemoration activity with a big crowd of people. In this period around the world, people are uniting to flatten the curve of COVID-19 infections and keep their neighbors safe. East African is thus no exception.

Continue Reading

Inaugural EAC Short Film Competition submission Portal now open

... total prize $25,000, submission deadline extended to 30th April 2020, and 33 youth winners to be selected.

March 30, 2020; Arusha, Tanzania: East African Community (EAC) has opened the portal for the submission of the inaugural Short Film Competition that was launched in January 2020.

Launched as part of the new drive to accelerate citizens engagement in year 2020, the maiden EAC Short Film Competition, is the latest efforts to inspire and capture views, and desires of the young citizens in East Africa. 

Continue Reading

EAC Secretariat to deploy mobile laboratories and testing kits and to all Partner States in a bid to mitigate Coronavirus

East African Community Headquarters, Arusha, Tanzania, 23rd March, 2020: The East African Community Secretariat is in the process of deploying mobile laboratories and Coronavirus test kits to all EAC Partner States.

Each Partner State will receive a four-wheel drive vehicle fitted with laboratory and ICT equipment, as well as all the necessary consumables for a fully functional laboratory with the capacity to conduct tests for Ebola and the coronavirus in addition to other pathogens.

Continue Reading

Frequently Asked Questions and Answers on COVID-19

Published 2nd April, 2020

In January 2020 the World Health Organization (WHO) declared the outbreak of a new coronavirus disease in Hubei Province, China, to be a Public Health Emergency of International Concern, as there was a high risk of the 2019 Coronavirus Disease (COVID-19) spreading to other countries around the world. As of 2nd April 2020, more than 896,450 cases have been confirmed in more than 200 countries, more than 45,526 people have died from the disease, but about 135,000 have also already recovered since the outbreak started. The EAC region did not stay unaffected and has to date confirmed cases in Burundi, Kenya, Rwanda, Tanzania and Uganda. Most infected people developed only mild symptoms and the average global death rate among confirmed cases of about 4 % is low compared to that of other infectious diseases which we are facing in the region, such as HIV/AIDS, Measles or Ebola. This rate might be almost 10 times higher than average for those over 80, and much lower for those under 40. Most affected by the pandemic is less the health sector, but the economy as a whole, including trade and tourism, as main life-lines in the region.

To succeed in combating the pandemic, all sections of our society including employers and businesses – must play a role and work together. The virus that causes the Coronavirus disease (COVID-19) is a new strain that had not been identified in humans until the outbreak of the disease in 2019.

Coronaviruses (CoV) are a large family of viruses that are common in animals and cause illness in humans ranging from a mild cold to more severe diseases such as the Middle East Respiratory Syndrome (MERS-CoV) and the Severe Acute Respiratory Syndrome (SARS-CoV).

Coronaviruses are zoonotic, meaning they are transmitted between animals and people. Detailed investigations found that SARS-CoV was transmitted from civet cats to humans and MERS-CoV from dromedary camels to humans. Other known coronaviruses are circulating in animals without causing illness in humans.

The COVID-19 outbreak has taken its toll on many countries worldwide and has caused huge economic losses with various sectors affected and impacted upon.

In the following we are providing answers to frequently asked questions regarding COVID-19:

+  What is a Coronavirus?

Coronaviruses are a large family of viruses which occur naturally in animals and may cause illness in animals and humans. In humans, coronaviruses cause respiratory infections ranging from common colds with mild symptoms to more severe diseases such as the Middle East Respiratory Syndrome (MERS) and the Severe Acute Respiratory Syndrome (SARS). The most recently discovered virus in this family causes the Coronavirus Disease, COVID-19.
 

+  What does COVID-19 stand for?

+  What is COVID-19?

+  What are the symptoms of COVID-19?

+  Who is most at risk of catching COVID-19?

+  Do I need to worry about my children?

+  How does COVID-19 spread?

+  How can I prevent myself from getting infected?

+  Which hygiene measures are effective?

+  Should I wear a facemask to protect myself against the virus?

+  What can I do to protect others if I am sick or have tested positive with the Coronavirus Disease?

+  Can someone who is released from COVID-19 quarantine still spread the disease?

+  How can I contribute to avoiding stigmatising people related to COVID-19?

+  Is there a treatment for COVID-19?

+  Is there a vaccine against COVID-19?

+  Must I fear COVID 19?

+  What can I do to ensure my workplace is safe for me and my colleague?

+  Is it safe to use public transport (Dalla Dalla or Matatu) with regard to COVID-19?

+  Can I attend the church service?

+  Are Africans less at risk of contracting the COVID-19 compared to other races?

+  Does eating bush meat pose a risk for COVID-19 infections?

+  Are patients who recovered from COVID-19 immune against the virus?

+  How safe are goods from China?

+  Can I get COVID-19 through second-hand clothes from overseas?

+  What is the difference between the average death rate among confirmed cases and the overall average death rate?

https://www.who.int/news-room/q-a-detail/q-a-coronaviruses

https://www.cdc.gov/coronavirus/2019-ncov/faq.html

Maswali ya Mara kwa Mara na Majibu kuhusu UVIKO-19

Imechapishwa Aprili 3, 2020

Mnamo Januari 2020 Shirika la Afya Duniani (WHO) lilitangaza mlipuko wa ugonjwa mpya wa virusi vya korona katika Mkoa wa Hubei, Uchina, kuwa suala la Hali ya Hatari ya Afya ya Umma Kimataifa kwa sababu ya uwezekano mkubwa wa Ugonjwa wa Virusi vya Korona vya mwaka 2019 (UVIKO-19) kuenea duniani kote. Kufikia Aprili 2 2020, wagonjwa zaidi ya 896, 450 wameambukizwa katika nchi zaidi ya 200, zaidi ya watu 45, 526 wamekufa kutokana na ugonjwa huo, lakini wengine 135,000 pia wametibiwa na kupona tangu kuzuka kwa ugonjwa huo. Katika Jumuiya ya Afrika Mashariki matukio ya ugonjwa huu wameripotiwa nchini Burundi, Kenya, Rwanda, Uganda na Tanzania. Watu wengi walioambukizwa huonyesha dalili zisizo kali na kiwango cha takribani 4% cha vifo ulimwenguni ni cha chini kikilinganishwa na magonjwa mengine ya kuambukiza yanayotokea ukanda huu kama vile VVU/UKIMWI, surua au Ebola. Janga hili  halijaathiri tu sekta ya afya, bali limeathiri uchumi kwa ujumla, ikiwa ni pamoja na biashara na utalii, ambazo ndio nguzo kuu za maisha katika ukanda huu.

Ili kufanikiwa katika kukabiliana na janga hili, makundi yote katika jamii yetu ikiwa ni pamoja na waajiri na wafanyabiashara – ni lazima yahusike na kushirikiana. Kirusi ambacho husababisha Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO-19) ni cha aina mpya ambacho hakikuwa kimewahi kutokea kwa binadamu hadi ugonjwa huo ulipozuka mwaka wa 2019.

Virusi vya Korona (ViKo) ni kundi kubwa la virusi ambavyo kwa kawaida hupatikana kwa wanyama na husababisha maradhi hatari yanyohusiana na upumuaji kama vile Dalili za Upumuaji za Middle East (Middle East Respiratory Syndrome (MERS-CoV) na Dalili Kali na Hatari za Upumuaji (Severe Acute Respiratory Syndrome (SARS- CoV).

Virusi vya korona huambukizwa baina ya wanyama na watu. Uchunguzi wa kina ulibaini kuwa virusi vikali na hatari vya SARS-CoV viliambukizwa binadamu kutoka paka aina ya ngawa navyo virusi vya upumuaji vya MERS-CoV viliambukizwa binadamu kutoka ngamia wenye nundu moja. Kuna virusi vya korona vingine vinavyojulikana kuwa vinapatikana miongoni mwa wanyama bila kusababisha ugonjwa kwa binadamu.

Mlipuko wa UVIKO-19 umeathiri vibaya nchi nyingi duniani na umesababisha hasara kubwa katiak sekta mbalimbali za kiuchumi.

Katika sehemu ifuatayo tunatoa majibu ya maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu UVIKO-19:

 

+  Virusi vya Korona ni nini?

Virusi vya korona ni kundi kubwa la virusi ambayvo kwa kawaida hupatikana miongoni mwa wanyama na vinaweza kusababisha ugonjwa kwa wanyama na binadamu. Kwa binadamu, virusi vya korona husababisha magonjwa ya kupumua kama vile homa ya kawaida isiyo na dalili kali na Dalili za Upumuaji za Middle East (Middle East Respiratory Syndrome (MERS) na Dalili Kali na Hatari za Upumuaji (Severe Acute Respiratory Syndrome (SARS). Virusi vilivyopatikana hivi karibuni husababisha Ugonjwa wa Virusi vya Korona, UVIKO-19.
 

+  Nini maana ya UVIKO-19?

UVIKO-19 ni kifupisho cha Ugonjwa wa Virusi vya Korona. Katika Kiingereza, UVIKO ni COVID (Corona Virus Disease). Katika kifupisho UVIKO-19, 'U' kinawakilisha 'Ugonjwa,' 'VI' 'Virusi,' na 'KO' ni Korona. Jina ‘COVID’ linafuata taratibu za Shirika la Afya Duniani (WHO) za kutaja magonjwa mapya ya kuambukiza kwa binadamu.
 

+  UVIKO-19 ni nini?

Ugonjwa wa Virusi vya Korona unafanana na homa ya mafua inayoambukizwa kwa kasi mno.
 

+  Nini dalili za UVIKO-19?

Dalili za kawaida za UVIKO-19 ni homa, uchovu, na kikohozi kikavu. Baadhi ya wagonjwa wanaweza kuwa na maumivu na uchungu, kubanwa pua, kutokwa kamasi, vidonda kooni au kuhara. Mara nyingi dalili hizi huwa si kali na huanza polepole. Watu wengine huambukizwa lakini hawaonyeshi dalili zozote na huwa hawajisikii vibaya. Watu wengi (takribani asilimia 80) hupona kutokana na ugonjwa huu bila kuhitaji matibabu maalum. Ni kama mtu mmoja kati ya watu sita wanaopata UVIKO-19 ndiye hudhoofika na kutatizika kupumua.
 

+  Ni nani aliye katika hatari kubwa zaidi ya kupata UVIKO-19?

Mtu yeyote anayekumbana na virusi vinavyosababisha UWIKO-19 yuko hatarini. Hata hivyo, watu wa umri mkubwa, na wale walio na hali nyingine za kiafya kama vile shinikizo la damu, magonjwa ya moyo na ugonjwa wa kisukari au wale ambao kinga ya mwili imedhoofika, kama vile watu walio na VVU/UKIMWI au saratani, wako katika hatari zaidi na wana uwezekano mkubwa wa kupata dalili kali.
 

+  Ninahitaji kuhofia watoto wangu?

Visa vya watoto kuambukizwa vimeripotiwa. Hata hivyo, watoto na hata vijana hawaonekani kuathiriwa sana na Ugonjwa wa Virusi vya Korona kama ilivyo kwa wazee.
 

+  UVIKO-19 husambaa vipi?

Ugonjwa huu unaweza kusambaa kutoka mtu mmoja kwenda mtu mwingine kupitia vitonetone wakati mtu aliyeambukizwa anapopiga chafya, anapokohoa au anapopumua. Wakati mwingine watu huambukizwa UVIKO-19 wanapogusa vitu au sehemu yenye virusi na kujigusa machoni, puani au mdomoni.
 

+  Ninaweza kujikinga vipi ili nisiambukizwe?

Njia bora ya kuzuia kuambukizwa ni kuepukana na kukumbana na virusi. Hili linawezekana kwa kuzingatia hali ya juu ya usafi, kuepuka kugusana na watu walioambukizwa na kujitenga na watu wengine kwa umbali wa futi 6, kwa sababu virusi hivyo husambaa mara nyingi kutoka mtu mmoja hadi kwa mwingine na baina ya watu waliokaribiana. Hili ni muhimu sana haswa kwa watu ambao wako katika hatari kubwa ya kuwa wagonjwa.
 

+  Ni hatua gani za usafi zilizo muafaka?

  • Safisha mikono yako mara kwa mara kwa kuiosha kwa sabuni na maji kwa angalau sekunde 20, haswa baada ya kuwa mahali pa umma, au baada ya kusafisha pua, kukohoa, au kupiga chafya.
    • Unaweza pia kutumia kitakasa mikono ambacho kina angalau asilimia 60 ya kileo. Sugua mikono yako mpaka ikauka.
    • Usijiguse machoni, puani na mdomoni kwa mikono isiyooshwa.

+  Ninahitaji kuvaa barakoa ili nijikinge na virusi hivi?

Huhitaji kuvaa barakoa kama wewe si mgonjwa au unamhudumia mgonjwa (ambaye hawezi kuvaa barakoa). Barakoa ziachiwe wale wanaozihitaji.
 

+  Ninaweza kufanya nini kuwakinga wengine iwapo mimi ni mgonjwa au nimepatikana na Ugonjwa wa Virusi vya Korona?

kiwa unaugua, usitoke nyumbani, isipokuwa pale unapohitaji huduma ya matibabu, hata kama haijathibitishwa kwamba umeambukizwa Virusi vya Korona au una homa ya kawaida. Pia:
  • Funika mdomo na pua kwa kitambaa wakati unapokohoa au kupiga chafya au fanya hivyo ndani ya kiwiko chako na ukioshe baadaye.

  • Tupa kifaa kilichotumika kwenye takataka.

  • Bila kuchelewa nawa mikono yako kwa sabuni na maji kwa angalau sekunde 20 au safisha mikono kwa kutumia kitakasa mikono chenye angalau silimia 60 ya kileo.

  • Vaa barakoa unapokuwa karibu na watu wengine (k.m. mnapotumia chumba kimoja au gari na kabla ya kuingia kwenye kituo cha afya.

  • Kwanza safisha halafu takasa kila siku sehemu zinazoguswa mara kwa mara, kama vile meza, vitasa vya milango, swichi za umeme, mipini, dawati, simu, kibodi, vyoo, bomba na sinki za maji.

+  Mtu aliyeachiliwa kutoka karantini ya UVIKO-19 anaweza kusambaza ugonjwa huo?

Mtu ambaye ameachiliwa kutoka karantini ya UVIKO-19 hana hatari ya kueneza virusi kwa sababu hakuonyesha dalili wakati wa kipindi alichokuwa amezuiliwa.

Maana ya karatinti ni kumtenga mtu (au kikundi cha watu) na watu wengine aliyekumbana na ugonjwa wa kuambukizwa lakini ambaye hajaonyesha dalili ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa huo.

Karantini kwa kawaida hutegemea urefu wa kipindi cha ugonjwa wa kuambukizwa, ambao ni muda wa watu kuonyesha dalili za ugonjwa. Kwa UVIKO-19 kipindi hiki ni siku 14 kutoka tarehe ya mwisho kukumbana na ugonjwa huu, kwa kuwa siku 14 ndicho kipindi kirefu zaidi cha kupevuka kinachoonekana kwa virusi vingine vya aina hii ya korona.

+  Ni kwa namna gani ninaweza kuchangia kuzuia unyanyapaa wa watu wenye virusi vya UVIKO-19?

Hofu na wasiwasi vinaweza kusababisha unyanyapaa-kijamii, kwa mfano, kwa watu waliokuwa karantini ya UVIKO-19. Unyanyapaa unatokana na kutokuwa na habari kamili kuhusu UVIKO-19 na jinsi unavyoenea au kutokana na udaku na uzushi. Unaweza kuzuia unyanyapaa na kusaidia wengine kwa kutoa msaada wa kijamii.

Unaweza kupigana na unyanyapaa na kuwasaidia, na siyo kuwadhuru, wengine katika jamii. Unaweza kupinga unyanyapaa kwa kujifunza na kuwafunza wengine ukweli, kwa mfano kwamba virusi havilengi makundi fulani ya jamii.

Toa taarifa mpya kuhusu UVIKO-19 kwa wenzako lakini epukana na kueneza uongo.
 

+  Kuna tiba ya UVIKO-19?

Hakuna tiba maalum ya UVIKO-19. Usiwaamini watu wanaojaribu kukuuzia dawa na kuahidi kwamba watauponya ugonjwa huo. Magonjwa ya virusi yanaweza kuzuiwa na chanjo ikipatikana, lakini hayawezi kuponywa kwa kutumia viuavijasumu. Hata hivyo, matibabu au tiba inaweza kusaidia kupunguza dalili zinazoambatana na virusi, kama vile homa au kikohozi.
 

+  Kuna chanjo dhidi ya UVIKO-19?

Kufikia sasa, hakuna chanjo dhidi ya UVIKO-19. Wagonjwa watapata msaada na uangalizi kutoka kwa wahudumu wa afya hadi watakapopona.
 

+  Ni lazima niogope UVIKO-19?

Kila ugonjwa wa virusi ni hatari na UVIKO-19 unaambukizwa kwa wepesi sana. Ugonjwa huu unaweza kuenea kwa haraka mno na kuambukiza watu wengi katika kipindi kifupi. Hata hivyo, dalili za UVIKO-19 mara nyingi huwa si za kutisha. Wagonjwa wengi huwa hawaonani na daktari. Kiwango cha asilimia 4 ya vifo vya UVIKO-19 kinachotokea ni cha chini kikilinganishwa na magonjwa mengine ambayo yanatokea katika ukanda huu. Kwa Mfano: Kiwango cha vifo vya ugonjwa wa surua au virusi vya Ebola kinaweza kuwa zaidi ya asilimia 60 na hadi asilimia 100 ya watu wanaoambukizwa kichaa cha mbwa watakufa.

Mfano mwingine: Nchi ya Uchina, yenye watu zaidi ya bilioni 1.4, ni watu 80,000 tu ambao wamethibitishwa kuwa na UVIKO-19.

+  Ninaweza kufanya nini kuhakikisha maeneo ya kazi ni salama kwangu na kwa wenzangu?

Ikiwa UVIKO-19 utafika kazini kwako, unaweza kusimamisha au kuzuia kuenea kwake kwa kupunguza siku za kufanya kazi:
  • Hakikisha umedumisha usafi kila sehemu kazini kwako (k.m. madawati na meza) na vitu (k.m simu, kibodi). Vifute na vitakasa mara kwa mara.

  • Himiza wafanyikazi na wageni kuosha mikono kwa makini mara kwa mara.

  • Hakikisha maeneo ya kazi yana nafasi za kutosha kuruhusu hewa safi kuzunguka (usafi mzuri wa kupumua).

+  Ni salama kutumia usafiri wa umma (Daladala au Matatu) kipindi hiki cha UVIKO-19?

Abiria katika Matatu au Daladala huwa wamesongamana na hakuna njia ya kutenga nafasi baina ya abiria mmoja na yule anayekohoa na kupiga chafya na kuzuia kusambaa kwa vitonetotone kutoka pua yake na mdomo wake. Kwa hivyo, utumiaji wa usafiri wa umma una hatari kubwa ya maambukizi ya UVIKO-19 na magonjwa mengine ya kuambukiza. Ikiwezekana, usafiri mbadala utumiwe kana njia ya kuzuia maambukizi wakati huu wa UVIKO-19.
 

+  Ninaweza kuhudhuria ibada?

Huu ni uamuzi wa kibinafsi. Kwa hakika, ibada inaweza kusaidia kuenea maambukizi kwa kuwa watu wengi hukusanyika na kukaa na kusimama karibu-karibu.Ukifikiri kuwa kuhudhuria ibada ni bora kuliko kujikinga dhidi ya UVIKO-19, basi huo utakuwa uamuzi wako binafsi. Ukiamua kuhudhuria ibada, jitenge na washiriki wenzako kadri iwezekanavyo na epuka kusalimiana. Unaweza pia kumhusisha kiongozi wako wa dini katika kulishughulikia janga hili. Ikiwa tayari una UVIKO-19, KAMWE usiende kwenye ibada, kwa kuwa utahatarisha usalama wa wenzako.
 

+  Waafrika wana kinga dhidi ya UVIKO-19?

Habari zisizo za kweli vimeanza kuibuka kuhusu UVIKO-19. Mojapo ni kwamba Waafrika wana kinga dhidi ya UVIKO-19. Usiamini habari kama hizo. Ugonjwa huu haumbagui mtu yeyote. Tayari zaidi ya nchi 35 za Afrika zimeripoti matukio ya visa vya UVIKO-19, uthibitisho kwamba hakuna usalama bila tahadhari na kujikinga.
 

+  Je, kula nyama ya mwituni kuna hatari ya maambukizi ya UVIKO-19?

Nyama ya mwituni inadhaniwa kuwa chanzo cha janga la sasa la virusi vya korona. Virusi vya korona na bakteria nyingine hujitokeza kwa kawaida katika wanyama. Kwa hivyo, mchakato wa kuandaa nyama ya kula unahitaji kufuata kanuni za maandalizi safi na salama ya chakula. Nyama inapaswa kukaguliwa na wataalam wanaohusika na watumiaji wanashauriwa kuiandaa vizuri, kwa kupika au kuikaanga ili iive na isiwe mbichi.
 

+  Wagonjwa waliopona kutokana na UVIKO-19 wana kinga dhidi ya virusi hivyo?

Ni mapema mno kutoa jubu la uhakika. Hata hivyo, kuna ushahidi wa kisayansi unaonyesha kuwa mtu aliyeambukizwa UVIKO-19 na kupona hujenga aina fulani ya kinga dhidi ya mbegu ya kirusi iliyosababisha maambukizi. Wanasayansi nchini Uchina kwa makusudi waliambukiza nyani aina ya ngedere UVIKO-19 na pia wakawaambukiz ngedere walionusurika kiwango kikubwa cha virusi. Hakuna ngedere aliyeambukizwa mara ya pili aliyekuwa mgonjwa. Mkabiliano wa kujikinga na maradhi wa ngedere unafanana kwa kiasi fulani na ule wa binadamu. Hivyo, wataalamu kwa makini wanafasiri matokeo ya jaribio hilo kumaanisha kuwa binadamu aliyepona UVIKO-19 akiambukizwa tena hawezi kuathirika sana..
 

+  Bidhaa kutoka Uchina ni salama?

Majaribio ya kisayansi yalionyesha kuwa virusi vinavyosababisha UVIKO-19 vinaweza kuishi kwa nguo au sehemu ya juu ya kitu kwa saa kadhaa, kutegema hali nyingine kama vile kiwango cha joto, unyevunyevu na kadhalika. Iwapo bidhaa kutoka Uchina vitakuwa vimechafuliwa na virusi huwa vinasafiri masafa marefu kabla kufika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Hivyo, itakuwa vigumu kwa virusi hivyo kuwa bado hai. Hata hivyo, ikiwa maana ya ‘bidhaa’ ni pamoja na wanyama hai walio na virusi, bila shaka maambukizi yanaweza kutokea. Hivyo, Uchina imeweka marufuku ya biashara ya kigeni ya wanyama wa mwituni.
 

+  Ninaweza kupata UVIKO-19 kwa nguo kuukuu kutoka ng’ambo?

Virusi vinavyosababisha UVIKO-19 vinaweza kuishi kwa nguo au sehemu ya juu ya kitu kwa saa kadhaa, kutegema hali nyingine kama vile kiwango cha joto au unyevunyevu. Hata hivyo, iwapo nguo kuukuu zilitoka ng’ambo, zilisafiri masafa marefu na zitakuwa zilisafishwa na kuwekwa dawa ya kuua viini vya maradhi kabla ya kuuzwa kama inavyopendekezwa na viwango vya biashara ya kimataifa. Kwa hali hii, ni vigumu kwa virusi kupatikana katika nguo kuukuu.
Ikiwa bado una shaka na unataka uhakika na kuwa salama kabisa, osha nguo hizo kwa kutumia sabuni ya unga kwenye maji moto ya digrii 60 au zaidi. Hii itaviua virusi.
 

https://www.who.int/news-room/q-a-detail/q-a-coronaviruses

https://www.cdc.gov/coronavirus/2019-ncov/faq.html

EALA suspends its 4th Meeting of the 3rd Session

…EALA Commission calls off 3-week Plenary meeting in Arusha, over COVID-19 threat

East African Legislative Assembly, Arusha, Tanzania: 17 March, 2020: The 4th Meeting of the 3rd Session of the 4th Assembly which was scheduled to commence tomorrow (March 18th, 2020), has been called off.

At its 45th Meeting held on Tuesday 17th March 2020, the EALA Commission noted with concern that the NOVEL CORONAVIRUS DISEASE (COVID-19), continues to spread at an alarming level globally, including within the East African Community region.

Continue Reading

All EAC Meetings suspended due to novel Coronavirus Pandemic

East African Community Headquarters, Arusha, Tanzania, 17th March, 2020: The East African Community has suspended with immediate effect all meetings due to the novel coronavirus outbreak.

In a letter to EAC Partner States Permanent/Principal/Under Secretaries dated 16th March, 2020, EAC Secretary General Amb. Liberat Mfumukeko says that the Community had noted with concern that the virus continues to spread across the entire globe with increasing speed to a number of African countries.

Amb. Mfumukeko’s letter was written in response to a request by Hon. Vincent Biruta, the Chairperson of the EAC Council of Ministers, who in a letter to the Secretary General dated 12th March, 2020, asked the Secretariat to do three things: To postpone the 21st EAC Summit until further notice; To hold all scheduled meetings by Videoconference, where possible, and; To postpone and suspend all other meetings and activities that require large gatherings.

Continue Reading

EAC mulls adopting French as an official language of the Community

…..as EAC and Government of the French Republic sign MoU

East African Community Secretariat, Arusha, Tanzania, 13th March, 2020: French could in the near future become an official language of the East African Community in addition to English.

This became apparent after the French government agreed to assist the EAC in conducting a study on the modalities to include French as an official language of the Community.

Continue Reading


East African Community
EAC Close
Afrika Mashariki Road
P.O. Box 1096
Arusha
United Republic of Tanzania

Tel: +255 (0)27 216 2100
Fax: +255 (0)27 216 2190
Email: eac@eachq.org